Waziri Mkuu Mstaafu, John Samuel Malecela yupo taabani, amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo.
Spika wa Bunge la Jmhuri ya Muungano wa Tanzania, Anna Makinda aliwatangazia wabunge leo kabla ya kuahirisha kikao cha asubuhi kuwa Malecela ni mgonjwa.
Alisema, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela haonekani bungeni kwa sababu Mzee Malecela ni mgonjwa.
Kilango ni mke wa ndoa wa mzee Malecela.
“Waheshimiwa wabunge kwa siku kadhaa mheshimiwa Anne Kilango haonekani, yupo anamuuguza mzee Malecela kwa sababu amefanyiwa upasuaji mkubwa wa moyo,” alisema spika leo.
Hata hivyo, Spika Makinda hakueleza hali ya Malecela inaendeleaje, kama ana nafuu ama la.
Chadema, CCM mwafaka Arusha
HATIMAYE mgogoro wa uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha umepata ufumbuzi baada ya pande zinazohusika kufikia muafaka wa kupokezana madaraka.
HABARI ZAIDI HAPA
HABARI ZAIDI HAPA
Polisi watinga Ikulu kupeleka malalamiko yao
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Ukonga jijini Dar es Salaam, wanaolinda makazi ya viongozi mbalimbali wakiwemo wastaafu, wametinga Ikulu na kupeleka malalamiko yao kwa njia ya barua wakidai posho zao za mwaka 2006.
HABARI KAMILI HAPA
HABARI KAMILI HAPA
Suala la Posho, CHADEMA wagawika, watatu wapinga
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeingia kwenye mgogoro baada ya baadhi ya wabunge kupandwa na hasira dhidi ya wenzao wanaoendesha kampeni ya kutaka posho za vikao kwa wabunge ziondolewe.Mkwaruzano huo iliibuka ndani ya kikao cha wabunge wa Kambi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema na Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe.
HABARI KAMILI HAPA
HABARI KAMILI HAPA
Kuchimba dawa uwanjani kisa vyoo hamna
Monday, 20 June 2011
WACHEZAJI na mashabiki wa Yanga waliokuwapo katika mchezo wa kirafiki ulioikutanisha timu hiyo na kikosi cha Ilala juzi Jumamosi waliamua kujisaidia aja ndogo katika moja ya kuta za Uwanja wa Kaunda kutokana na uhaba wa vyoo.
Championi Jumatatu lilishuhudia idadi kubwa ya wachezaji wa Yanga wakijisaidia katika ukuta wa uwanja huo bila kujali lolote kwani hapakuwa na choo jirani na sehemu hiyo ya kuchezea. Vyoo vipo katika jengo la klabu hiyo mita chache kutoka uwanjani.
Inapotokea mchezaji au shabiki akakumbwa na haja, hatoweza kwenda katika jengo la klabu kujisaidia kutokana na umbali uliopoa pia kupata shida ya kuingia na kutoka katika geti kuu.
Licha ya Yanga kusifika kuwa na uwanja wake binafsi, kitendo cha Uwanja wa Kaunda kukosa choo huku ukitumika kwa mechi za kirafiki za timu hiyo, kinaiondolea sifa klabu hiyo ambayo ni mabingwa wa soka Tanzania Bara.
Akizungumza na gazeti hili uwanjani hapo, Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema umati uliofurika katika mchezo wao dhidi ya Ilala ulioisha kwa suluhu umeipa faraja klabu yake na kupata hamu ya kuutumia uwanja huo kwa mechi zake za kirafiki, kwani kila shabiki alilipa Sh 3000.
Hata hivyo, Sendeu alikiri kuwepo kwa kasoro ndogo ndogo katika uwanja huo.
Championi Jumatatu lilishuhudia idadi kubwa ya wachezaji wa Yanga wakijisaidia katika ukuta wa uwanja huo bila kujali lolote kwani hapakuwa na choo jirani na sehemu hiyo ya kuchezea. Vyoo vipo katika jengo la klabu hiyo mita chache kutoka uwanjani.
Inapotokea mchezaji au shabiki akakumbwa na haja, hatoweza kwenda katika jengo la klabu kujisaidia kutokana na umbali uliopoa pia kupata shida ya kuingia na kutoka katika geti kuu.
Licha ya Yanga kusifika kuwa na uwanja wake binafsi, kitendo cha Uwanja wa Kaunda kukosa choo huku ukitumika kwa mechi za kirafiki za timu hiyo, kinaiondolea sifa klabu hiyo ambayo ni mabingwa wa soka Tanzania Bara.
Akizungumza na gazeti hili uwanjani hapo, Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu alisema umati uliofurika katika mchezo wao dhidi ya Ilala ulioisha kwa suluhu umeipa faraja klabu yake na kupata hamu ya kuutumia uwanja huo kwa mechi zake za kirafiki, kwani kila shabiki alilipa Sh 3000.
Hata hivyo, Sendeu alikiri kuwepo kwa kasoro ndogo ndogo katika uwanja huo.
Summer Summer Summer time... Mishkakiiizzz
WANAFUNZI TOKA KENYA, UGANDA, TANZANIA, SWAZILAND, GHANA, N.K. WA CHUO KIKUU CHA URAFIKI LUMUMBA MOSCOW RUSSIA WAKIWA KATIKA MSITU ULIOPO KARIBU NA CHUO HICHO WAKIWA WANACHOMA MISHKAKI. INAPENDEZA WATU WA NCHI MBALIMBALI WAKIKAA PAMOJA
MISHKAKI IKIWA INAANDALIWA
KUTOKA KULIA WANAFUNZI WA KWANZA, WA PILI, WA TANO NA WA SITA WATANZANIA, WA TATU - NIGERIA NA WA NNE - ZAMBIA KATIKA POZI
SHUGHULI IKIWA INAENDELEA
WENZETU HUSEMA KAZI NA SALA, . uh...
wadau katika pozi
UDSM Honorary Degrees Awarded
KATIKA PITA PITA NIMEKUTANA NA HII, SAFI SANA UDSM... HONORARY DEGREE AWARD HAZITOKI OVYO OVYO KAMA PIPI....
/N | NAME | DEGREE | DATE/YEAR |
Degrees of the University E. A (Dar es salaam) | |||
1 | Prof. Karl Worth Bigelow | Doctor of Literature(honoris causa) | 1970 |
2 | Hon. Solomon Nkya Eliufoo | Doctor of Laws(honoris causa) | 1970 |
3 | Edward Walter Russell | Doctor of Science(honoris causa) | 1970 |
Degrees Awarded by UDSM | |||
4 | Hon. Justine Philip Telford | Doctor of Laws(LL.D) | 1973 |
5 | Hon. Abdulkarim Yusufali Alibair Karimjee | Doctor of Laws(LL.D) | 1973 |
6 | Hon. Aboud Jumbe Mwinyi | Doctor of Laws(LL.D) | 1976 |
7 | Hon. Adam Sapi Mkwawa | Doctor of Laws(LL.D) | 1980 |
8 | Hon. Amir H Jamal | Doctor of Literature(D. Litt) | 1980 |
9 | Dr. W K Chagula | Doctor of Science(honoris causa) | 1981 |
10 | Dr. Basil Risbridger Davidson | Doctor of Literature(D. Litt) | 1985 |
11 | Mwalimu Julius Kambarage Nyerere | Doctor of Literature(D. Litt) | 1986 |
12 | Dr. G .L Monekosso | Honorary Doctor Of Science(honoris causa) | 1989 |
13 | Prof. Tormod Forland | Honorary Doctor Of Science(honoris causa) | 1990 |
14 | Ambassador Amon James Nsekela | Doctor of Literature(D. Litt) | 1990 |
15 | Professor Dr. Ir.Godfried D.Vogels | Honorary Doctor Of Science(honoris causa) | 1998 |
16 | Ambassador J.V Mwapachu | Doctor of Literature(honoris causa) | 2005 |
17 | Hon B.W Mkapa | Doctor of Literature(honoris causa) | 2006 |
18 | Prof. Sven Erick Jorgensen | Doctor of Science(honoris causa) | 2007 |
NATO yakiri ilifanya makosa
Sunday, 19 June 2011
Wakaazi wa Tripol wakiangalia uharibifu uliofanywa na jeshi la NATO kwenye makaazi ya Raia
Moshi Mkubwa ukifuka juu baada ya shambulio la nato katika makaazi ya Raia
NATO imekubali kuwa "matatizo ya mtambo wa silaha" huenda yalisababisha mashambulio dhidi ya raia Jumapili asubuhi mjini Tripoli,Libya.
Katika taarifa,muungano huo wa majeshi umesema kuwa lengo ilikuwa ni kituo cha makombora cha kijeshi,lakini "inaonekana moja ya silaha"haikulenga kituo hicho.
Awali serikali ya Libya ilisema kuwa Nato imeshambulia eneo la makaazi ya watu,na kuwaua raia tisa,wakiwemo watoto.
Nato inatekeleza makubaliano ya Umoja wa Mataifa kuwalinda raid wa Libya kutoka kwa vikosi vinavyomuunga mkono Gaddafi.
'Familia ilishambuliwa'
"Nato inajutia kufarikia dunia kwa raia na inachukua hatua za makini katika kushambulia utawala ambao unatumia nguvu dhidi ya raia wake wenyewe," alisema Luteni Jenerali Charles Bouchard, kamanda wa harakati hizo.
" Ingawa bado tunachunguza sababu za tukio hili,ishara zinaonyesha kuwa ni matatizo ya mtambo wa silaha huenda yakawa sababu ya tukio lenyewe,"aliongeza.
Taarifa hio ilisema kuwa mashambulio zaidi ya 11,500 yamefanywa na "kila shambulio linapangwa na kutekelezwa kwa makini ili kuepuka mauaji ya raia".
Moshi Mkubwa ukifuka juu baada ya shambulio la nato katika makaazi ya Raia
NATO imekubali kuwa "matatizo ya mtambo wa silaha" huenda yalisababisha mashambulio dhidi ya raia Jumapili asubuhi mjini Tripoli,Libya.
Katika taarifa,muungano huo wa majeshi umesema kuwa lengo ilikuwa ni kituo cha makombora cha kijeshi,lakini "inaonekana moja ya silaha"haikulenga kituo hicho.
Awali serikali ya Libya ilisema kuwa Nato imeshambulia eneo la makaazi ya watu,na kuwaua raia tisa,wakiwemo watoto.
Nato inatekeleza makubaliano ya Umoja wa Mataifa kuwalinda raid wa Libya kutoka kwa vikosi vinavyomuunga mkono Gaddafi.
'Familia ilishambuliwa'
"Nato inajutia kufarikia dunia kwa raia na inachukua hatua za makini katika kushambulia utawala ambao unatumia nguvu dhidi ya raia wake wenyewe," alisema Luteni Jenerali Charles Bouchard, kamanda wa harakati hizo.
" Ingawa bado tunachunguza sababu za tukio hili,ishara zinaonyesha kuwa ni matatizo ya mtambo wa silaha huenda yakawa sababu ya tukio lenyewe,"aliongeza.
Taarifa hio ilisema kuwa mashambulio zaidi ya 11,500 yamefanywa na "kila shambulio linapangwa na kutekelezwa kwa makini ili kuepuka mauaji ya raia".
Askofu KKKT ajitosa mjadala wa posho
Mgeni rasmi katika mahafali ya 40 ya chuo cha Uuguzi Machame,mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe akizindua bweni la chuo hicho.
Mgeni rasmi katika mahafali ya 40 ya chuo cha uuguzi Machame,Mh Freeman Mbowe katikati akiimba wimbo wa taifa,kushoto kwake ni Baba askofu wa KKKT dayosisi ya kaskazini Martin Shao na kulia kwake ni kaimu mkurugenzi wa hospitali ya Machame,Masawe.
Mgeni rasmi katika mahafali ya 40 ya chuo cha uuguzi Machame,Mh. Freeman Mbowe akihutubia wananchi.
Baba askofu wa KKKT dayosisi ya kaskazini Martin Shao akihutubia wakati wa sherehe za mahafali ya 40 ya chuo cha uuguzi Machame.
Wahitimu.
Wazazi na wageni mbalimbali walifika kuhudhuria sherehe ya mahafali ya 40 ya chuo cha uuganga na uzinduzi wa bweni uliofanyika mwishoni mwa wiki katika hospitali ya Machame.
Na Dixon Busagaga,Hai.
KANISA la Kiinjili la Kilutheria Tanzania (KKKT) limeunga mkono hoja ya wabunge wa kambi ya upinzani kutaka wabunge na wafanyakazi wa kada za menejimenti za utumishi wa umma kutolipwa posho zisizo na tija na badala yake zipelekwe kwa matabibu,wauguzi na walimu wanaofundisha katika mazinira magumu vijijini.
Askofu wa kanisa hilo dayosisi ya Kaskazini Dkt Martin Shao aliyasema hayo katika mahafali ya 40 ya chuo cha uganga machame wilayani Hai yaliyokwenda sanjari na uzinduzi wa bweni la chuo cha uuguzi na harambee ya kuchangia ujenzi wa majengo ya chuo hicho.
Dkt Shao alisema wanaunga mkono juhudi za wabunge hao na kwamba ni vyema posho hizo zikatumika kuboresha maisha ya wafanyakazi wa kada za chini wakiwamo madaktari, wauguzi, wataalamu wengine wa elimu na wahudumu wa ofisi.
“Nchi hii kuna uozo ulioko huko wa kutanguliza mambo binafsi,umimi kwanza ,mimi naunganika na wale wanaosema posho hizo ziende zikasaidie maeneo mengine na wenzetu wanaotoa huduma kwa wengine katika mazingira magumu”alisema askofu Shao.
Dkt Shao alienda mbali zaidi huku akinukuu vifungu katika biblia,ambapo katika kitabu cha Wafilipi 2;3,4, alisema yapo maneno yanayosema “Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno bali kwa unyenyekevu ,kila mtu na amuhesabu mwenzie kuwa bora kuliko nafsi yake.
Aliongeza kuwa katika mstari wa nne katika kitabu hicho kinaendelea kusema kuwa kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe bali kila mtu aangalie mambo yaw engine huku akiwataka waheshiwa kushughulika na mambo ya wengine bila kutanguliza ubinafsi.
Aidha askofu Shao aliiomba serikali kupanga madaktari bingwa na wauguzi katIka hospitali za vijijini kwani asilimia 80 ya watanzania wanaishi vijiji hivyo wanahitaji huduma kikamilifu kwa kuwa ni haki kupata huduma hizo.
Aliwataka wauguzi kuacha tabia ya kutanguliza maslahi binafsi katika utoaji wa tiba bali kuzingatia viapo vyao jambo ambalo litawajengea heshima na utoaji wa huduma bora huku serikali na wadau wengine wakijitahidi kufikiri namna ya kuboresha maslahi yao.
Kwa upande wake mbunge wa Hai,Freeman Mbowe aliyekuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo alisema suala la Posho linaweza kuwatoa roho maana wamegusa mahali pabaya lakini hawaogopi kuendelea na mapambano kuhusu kupunguzwa kwa posho kwa kada mbalimbali za uongozi.
Alisema kwa mujibu wa uchunguzi aliofanya, nchi inatumia zaidi ya bil 912 kwa ajili ya kulipana posho kwa viongozi wa kada zote za utawala lakini kada nyingine zinaendelea kuwa masikini.
“Kilio chetu ni posho ambayo wanaonufaika ni viongozi wa ngazi za juu pekee ,huku wafanyakazi wa ngazi za chini kama walimu, wauguzi, madaktari,wahudumu wa ofisi,madereva na wengine ambao hawana uwezo wa kuitisha vikao hivyo wakiendelea kuwa masikini.”alisema Mbowe.
Hata hivyo alisema kambi ya upinzania haina pingamizi na Posho ya kujikimu ya 80,000 na ile ya kusafiri nje ya nchi wanazolipwa wabunge kwani ni halali,lakini tatizo lao posho hata kwa kazi ambazo hazipaswi kulipwa kwa kuwa ni sehemu ya wajibu.
Katika harambee ya ujenzi huo zilichangwa zaidi ya Sh mil 44 zikiwemo fedha taslimu na ahadi ambapo mbunge huyo alichangia Mil 10 huku kiasi kinachohitajika ni Mil 70.
Subscribe to:
Posts (Atom)















