CCM yazitakia heri Vijana U-23 na Simba SC katika michezo yao kesho

Saturday 18 June 2011

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
Vijana U-23
Simba SC


Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimezitakia  kila la kheri na kuibuka na ushindi timu za Simba na Timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 23  ambazo zinakabiliwa na mechi muhimu Jumamosi hii. 



Wakati  Simba itashuka dimbani na Motema Pembe katika mechi ya marudiano ya  kombe la shirikisho nchini Congo-DRC,  timu ya Vijana ya U-23 itashuka dimbani na vijana wenzao nchini  Nigeria katika mechi muhimu  ya kuwania kufuzu  kucheza fainali za Olimpiki.



Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM) Nape  Nnauye  imesema  kutokana na mechi hizo kuwa muhimu kwa timu hizo na pia kwa Watanzania, yeye binafsi na kwa niaba ya CCM anazitakia kila la heri timu hizo.



“CCM inependa kuona timu hizo zinafanya vizuri na kurejea na ushindi kwa  kuwa itakuwa ni ishara ya Tanzania kuimarisha ki-soka na hivyo kuwa mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM katika kuinua michezo nchini” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

0 comments:

Post a Comment