jaji mkuu azindua kampeni ya kuhamasisha utii wa sheria bila kushurutishwa leo

Saturday 18 June 2011

IDADI YA WATU WALIOSOMA HABARI HII: counter
 JAJI MKUU  MH. MOHAMED CHANDE OTHMAN (SHOTO) AKIZINDUA KAMPENI HIYO JIJINI DAR ES SALAAM LEO MCHANA
 JAJI MKUU MH. MOHAMED CHANDE OTHMAN CHANDE AKIHUTUBIA WAKATI  AKIZINDUA KAMPENI HIYO JIJINI DAR ES SALAAM LEO MCHANA
WADAU MBALIMBALI WAKIFUATILIA UZINDUZI HUO
 IGP-SAID MWEMA AKITOA HOTUBA YAKE
 
ASKARI WA JESHI LA POLISI WAKISOMA UTENZI
WADAU WALIOSHIRIKI UZINDUZI WA KAMPENI YA JESHI LA POLIS YA UTII WA SHERIA BILA SHURUTI

JAJI Mkuu Mh. Mohamed Chande Othaman amewataka wananchi kutii sheria bila kushurutishwa kwani kufanya hivyo kutavisaidia vyombo vya utoaji haki kutekeleza majukumu yake kwa ufasaha na ufanisi zaidi.



Aliongeza kuwa kwa kufanya hivyo pia  kutaiwezesha  jamii kuishi kwa amani, usalama na utulivu pamoja na kupunguza hali ya watu kuishi kwa mashaka na wasiwasi, kupunguza matumizi ya nguvu na kuimarika kwa mahusiano ya kiutendaji  kati ya vyombo vya dola na wananchi.


"Kwa jumuiko hili ambalo linashirikisha vyombo na wadau wakuu wa utoaji na usimamizi wa haki, ninathubutu  kusema kuwa kampeni hii nimeipokea kwa moyo mmoja na ninaamini kwamba tutashirikiana kwa chachu ya utekelezaji wa mkakati huu kwa vitendo kwa kuwa hakuna mtu aliye juu ya sheria".


Aidha ametoa wito kwa taasisi za kiserikali na zisizokuwa za kiserikali kujumuika pamoja  katika kampeni hii ya kuhamasisha wananchi kutii sheria bila kushurutishwa.

0 comments:

Post a Comment